Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kauli ya ‘usifanye hiki usifanye kile’ inadidimiza ndoto za wasichana – Frida Amani

Kauli ya ‘usifanye hiki usifanye kile’ inadidimiza ndoto za wasichana – Frida Amani

Pakua

Makala hii inakupeleka Nairobi, Kenya ambako Priscilla Lecomte wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Mratibu wa hatua dhidi ya majanga ya tabianchi na El Niño anazungumza na Mwanamuziki Frida Amani wa Tanzania. Frida Amani anatoa wito kwa watoto wa kike duniani kutokatishwa tamaa kwa kuambiwa “usifanye shughuli fulani kwa kuwa ni ya kiume” kwani kama yeye angekata tamaa asingeweza kuwa msanii wa Hip Hop ambayo imemfikisha katika majukwaa ya kimataifa kiasi cha kuandaa wimbo wa kuhamasisha ushirikiano wa kimataifa katika kuchukua hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi, wimbo ambao umeungwa mkono na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira Duniani (UNEP). Hapa Frida anaanza kwa kueleza kwa nini wimbo alioshirikiana na msanii Dex Mc Bean wa Marekani waliamua kuupa jina Twende na Mpango.

Audio Credit
Flora Nducha/Priscilla Lecompt
Audio Duration
3'8"
Photo Credit
UNEP