Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mlo shuleni umeongeza idadi ya wanafunzi wangu shule ya Salama: Mwalimu Beatrice Nyakoa Osaka

Mlo shuleni umeongeza idadi ya wanafunzi wangu shule ya Salama: Mwalimu Beatrice Nyakoa Osaka

Pakua

Shule ya Salama iliyo katika eneo la Huruma karibu na mtaa wa mabanda wa Mathare jijini Nairobi Kenya hivi karibuni imeanza programu ya mlo shuleni kupitia mradi wa kampuni ya ‘Food for Education”. Hatua hiyo imenfa idadi ya wanafunzi wanaosoma shule hiyo kuongezeka kutoka 1, 900 hadi 2,300. Mlo shuleni ni moja ya masuala ambayo yanapigiwa debe kubwa na Umoja wa Mataifa sio tu kwa sababu ya kuhakikisha lishe bora kwa mamia ya maelfu ya wanafunzi ambao wengi hawawezi kupata mlo nyumbani bali pia kuongeza idadi ya watoto wanaohudhuria masomo. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini Kenya UNIS Nairobi amefunga safari hadi shuleni Salama na kuzungumza na mwalimu mkuu wa shule hiyo Beatrice Nyakoa Osaka anayeenza kwa kufafanua umuhimu wa mradi huo shuleni kwake hasa kutokana na eneo walipo.

Audio Credit
Assumpta Massoi/Flora Nducha
Audio Duration
6'7"
Photo Credit
UNIS/Stella Vuzo