Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mchango wa wanawake katika kulinda mazingira ni wa thamani sana: Dkt. Josephine Ojiambo

Mchango wa wanawake katika kulinda mazingira ni wa thamani sana: Dkt. Josephine Ojiambo

Pakua

Katika kuelekea siku ya wanawake duniani ambayo itaadhimishwa Ijumaa wiki hii Machi 8 mchango wa wanawake katika kulinda na kuhifadhi mazingira umeelezwa kuwa ni mkubwa na wa thamani sana. Kandoni mwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Baraza la mazingira duniani UNEA6 uliofanyika Nairobi Kenya na kukunja jamvi mwishoni mwa wiki, nada mbalimbali zilijadiliwa ikiwemo mchango wa wanawake. Stella Vuzo afisa habari wa kitengo cha habari cha Umoja wa Mataifa Nairobi UNIS alizungumza na Balozi na mtafiti katika Mradi wa Green Transition nchini Kenya Dkt. Josephine Ojiambo kuzungumzia mchango huo wa wanawake katika kulinda mazingira.

Audio Credit
Anold Kayanda/Stella Vuzo
Audio Duration
3'57"
Photo Credit
© UNEP / Kiara Worth