Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Kampeni ya UNDP Tanzania ya kukabili misimamo mikali yainua vijana kiuchumi Kilwa Masoko mkoani Lindi

Kampeni ya UNDP Tanzania ya kukabili misimamo mikali yainua vijana kiuchumi Kilwa Masoko mkoani Lindi

Pakua

Nchini Tanzania, shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Maendeleo, UNDP linatekeleza mradi wa kukabili misimamo mikali kupitia kampeni ya amani kama njia mojawapo ya kufanikisha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs. Tayari kuna wanaufaika na mmoja wao ni Nuru Mbaruku Ramadhani, mwenyekiti wa kikundi cha Masoko 2 Peace Club kilichoko Kilwa Masoko mkoa wa Lindi, kusini mashariki mwa Tanzania. Kikundi hiki kilichoanzishwa mwezi Juni mwaka 2023, kina mabalozi 9 wa amani wakiwemo wanawake 6 na wanaume 3. Nuru akizungumza na Sawiche Wamunza, Afisa mchambuzi wa mawasiliano UNDP Tanzania anaaanza kuelezea kwa nini walianzisha kikundi hiki.

Audio Credit
Anold Kayanda/Evarist Mapesa
Sauti
5'1"
Photo Credit
UNDP/Tanzania