WHO na wadau waingilia kati kupambana na utapiamlo mkali unaosababishwa na athari za ukame Pembe ya Afrika
Pakua
Ukame katika ukanda wa Pembe ya Afrika umeleta madhara makubwa kwa ustawi wanadamu na ikolojia nzima katika eneo hilo. Madhara ya moja kwa moja yaliyoshuhudiwa na watu wa ukanda huo zikiwemo nchi za Somalia, Kenya, Ethiopia na maeneo ya kaskazini mwa Uganda ni ukosefu wa chakula na hivyo kusababisha utapiamlo hasa utapiamlo mkali kwa watoto.
Mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo la Afya Ulimwenguni, WHO na wadau wake, wameingilia kati ili kupunguza makali ya tatizo hilo kama si kulimaliza kabisa. Anold Kayanda ameangazia hatua hizo na kutuandalia makala ifuatayo.
Audio Credit
Selina Jerobon/Anold Kayanda
Audio Duration
3'3"