Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Zambia: FISH4ACP kusaidia uvuvi endelevu wa dagaa Kapenta na samaki buka

Zambia: FISH4ACP kusaidia uvuvi endelevu wa dagaa Kapenta na samaki buka

Pakua

Nchini Zambia, wafanyabiashara ya samaki kandokando ya Ziwa Tanganyika wameanza kuwa na wasiwasi kuwa uvuvi usizingatia kanuni za uvuvi bora unaweza kuhatarisha ustawi wao ambao unategemea biashara ya dagaa aina wafahamikao nchini humo kama Kapenta na samaki aina ya Buka.

Ili kuondokana na hali hiyo, hapo ndipo unapoingia Mradi wa FISH4ACP ambao ni mkakati wa shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO kwa kushirikiana na Muungano wa Afrika, AU na ule wa nchi za Karibea na Pasifiki OACPS, kuhakikisha minyororo ya thamani ya uvuvi na ufugaji wa samaki barani Afrika, Karibea na Pasifiki kuwa endelevu zaidi. Anold Kayanda na maelezo zaidi kupitia makala hii.

Audio Credit
Leah Mushi/Anold Kayanda
Audio Duration
3'57"
Photo Credit
Picha: FAO/Oumou Khaïry Ndiaye