IOM yasaidia kuwarejesha nyumbani raia wa Sudan Kusini
Pakua
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linasaidia maelfu ya raia wa Sudan Kusini kurejea nyumbani.
Kwa mujibu wa shirika hilo maelfu ya raia hao wengi walikuwa wamekwama katika eneo la Kosti na wengine ni wale walioishi Kaskazini kwa muda na sasa wanataka kurudi nyumbani.
Hata hivyo IOM inasema licha ya kuanza kuwasafirisha watu hao ni zoezi litakalochuka muda mrefu na linahitaji fedha, ingawa kiasi wamefanikiwa kama anavyofafanua Jumbe Omari Jumbe afisa wa shirika hilo.