Elimu Tanzania yakabiliwa na changamoto
Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO kuhusu elimu kwa wote ambalo ni lengo namba mbili la Milenia, imebaini kuwa kasoro katika sekta ya elimu hugharimu serikali duniani kote dola Bilioni 129 kwa mwaka. Hii ni kwasababu asilimia 10 ya fedha zinazoelekezwa kwenye elimu ya msingi hupotelea kwenye kiwango duni cha elimu ambacho hakiwawezeshi watoto kufuta ujinga wa kutokujua kusoma.