Mtandao thabiti wa Intaneti kutaimarisha ukuaji jumuishi na endelevu Afrika. UN
Nchi za Afrika zimechagizwa kuwekeza katika kujenga mnepo wa miundombinu thabiti ya ya mtandao wa intaneti ili kutumia fursa za kidijitali na kuharakisha mageuzi ya kijamii na kiuchumi barani humo.
Hayo yameelezwa na viongozi wa kimataifa wanaohudhuria kongamano la 17 la udhibiti wa mtandao IGF 2022 linalofanyika Addis Ababa, Ethiopia, wakisisitiza umuhimu wa teknolojia ya kidijitali kama zana za kuimarisha maendeleo kote barani Afrika.