Ubaguzi wa kimfumo dhidi ya watu wenye asili ya Afrika bado kutokomezwa
Hatua za kutokomeza ubaguzi wa kimfumo dhidi ya watu wenye asili ya Afrika zinatekelezwa vipande vipande licha ya serikali mbalimbali duniani kutangaza hatua za kumaliza kitendo hicho dhalimu, imesema ripoti ya Umoja wa Mataifa itakayowasilishwa mbele ya Baraza la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu Jumatatu ijayo. Leah Mushi na maelezo Zaidi.
Ushiriki mapema wa baba na mama kwenye malezi ya mtoto waongeza uelewa wa mtoto
Nchini Zambia wakazi wa kijiij cha Kholowa wilaya ya Katete jimbo la Mashariki wameanza kuona manufaa ya mradi wa maendeleo ya mapema ya mtoto, ECD unaotekelezwa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF, mradi ambao alianza mwaka 2018 na unashirikisha baba na mama katika malezi ya mtoto tangu akiwa tumboni mwa mama yake hadi anapozaliwa na anapoendelea kukua. Taarifa ya Assumpta Massoi inafafanua zaidi.
Nyumbani kwa Posilio Phiri akisema UNICEF ilianza kwa kutufundisha jinsi ya kucheza na mtoto akiwa tumboni mwa mama yake.
Ubaguzi, unyanyasaji pahala pa kazi pamoja na COVID-19 vyatikisa afya ya akili ya wafanyakazi- Ripoti
Hatua Madhubuti zinahitajika ili kukabiliana na changamoto za afya ya akili miongoni mwa wafanyakazi , kwa mujibu wa wito mpya wa pamoja uliotolewa leo na shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni WHO na lile la kazi duniani ILO. Taarifa ya Anold Kayanda inafafanua zaidi.
Mradi wa zaidi ya dola milioni 9 kuimarisha mimea na usalama wa chakula wazinduliwa na FAO Tanzania
Katika kutekeleza lengo namba 15 la Maendeleo endelevu kuhusu kuimarisha uhai wa viumbe vya nchi kavu Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO) kwa kushirikiana na Muungano wa Ulaya, (EU) limezindua mradi wa kuimarisha Huduma za Afya ya Mimea na usalama wa chakula nchini Tanzania.
Afisa Afya ya Mimea kutoka FAO, Mushobozi Baithani anasema lengo la mradi huo ni kuboresha sekta ya mimea na mazao pamoja na kutatua changamoto kwa wafanyabiashara.
Jumuiya ya kimataifa inapaswa kuangazia zaidi mwelekeo wa mkataba wa amani Sudan Kusini
Jumuiya ya kimataifa inapaswa kuangazia zaidi na kwa mwelekeo wa mkataba wa amani Sudan Kusini pamoja na ongezeko la ghasia miongoni mwa jamii nchini kote Sudan Kusini, wameonya wataalamu wa Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu nchini humo baada ya kuhitimisha ziara yao jijini New York, Marekani ambako wamepata fursa ya kuzungumza na maafisa mbalimbali. Assumpta Massoi na maelezo zaidi.
Kipindi cha mpito Burkina Faso tunachukua hatua kurejesha utulivu- Rais Damiba
Mjadala Mkuu wa mkutano wa 77 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA77 ukiwa umeingia siku ya nne hii leo, Rais Paul Damiba wa Burkina Faso amesema tayari wamejiwekea mpango mkakati wa kurejesha utulivu nchini mwake wakati huu ambapo anaongoza serikali ya mpito kuanzia kufuatia mapinduzi ya kijeshi ya mwezi Januari mwaka huu.
Rais Damiba amesema hali ya usalama Burkina Faso alianza kuzorota mwaka 2015 na kilele kufikia mwaka 2020/2021 hali iliyosababisha changamoto kama vile ukimbizi wa ndani, kutwama kwa shughuli za kiuchumi.
Baada ya kunusurika kuozwa kisa ukame, mtoto 'Carol' sasa aomba asaidiwe aende shule
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limesema watoto wengi na hususan wa kike katika jamii zilizoathirika na ukame nchini Kenya ikiwemo Turkana wako katika hatari hasa ya kuozwa mapema kwa sababu familia nyingi zinahaha kuweka mlo mezani na suluhu ya karibu wanayoiona ni kuoza binti zao mapema ili kujikimu. Sasa shirika hilo linashirikiana na mamlaka za huduma ya ulinzi kwa watoto katika maeneo yaliyoathirika ili kuwalinda dhidi ya ajira ndoa za utotoni. Mary Kabora na maelezo zaidi.
Kando ya UNGA77, viongozi wa nchi wakutana kujadili magonjwa yasiyoambukiza
Shirika la afya la Umoja wa Mataifa ulimwengiuni WHO leo kandoni mwa mjadala wa wazi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaoendelea mjini Newy York Marekani limezindua ripoti mpya inayowataka viongozi wa dunia kuchukua hatua za haraka dhidi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza NCDs ambayo hukatili Maisha ya watu milioni 17 kila mwaka. Leah Mushi na taarifa Zaidi
Kiu ya kutafuta nishati salama nyumbani ilisababisha kubuni matumizi ya betri chakavu kutengeneza nishati
Kijana Gibson Kawago kutoka Tanzania ambaye ni miongoni mwa vijana 17 walioteuliwa na Umoja wa Mataifa kuwa viongozi vijana wa kusongesha malengo ya maendeleo endelevu, SDGs amesema atatumia kipindi cha miaka miwili cha nafasi hiyo kusongesha hatua kwa tabianchi ikiwemo kutumia ugunduzi wake kuchakata betri chakavu za kompyuta kutengeneza betri za kuzalisha umeme katika kulinda na kuhifadhi mazingira.
Nina furaha sana kuteuliwa na nitakuwa balozi mwema