Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

©UNICEF/Bernardino Soares

Wanawake wanaotumia intaneti ni asilimia 57 tu duniani ikilinganishwa na asilimia 62 ya wanaume-ITU

Katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya wasichana katika tasnia ya Habari na teknolojia ya mawasiliano ICT muungano wa kimataifa wa mawasiliano ITU umesema fursa na usalama mtandaoni ambayo ndio maudhui ya siku ya mwaka huu ni ufunguo wa kukiingiza kizazi kijacho cha wasichana katika Habari na teknolojia ya mawasiliano.

Sauti
2'50"
UN

Wazazi wasione aibu kuwaelimisha watoto kuhusu afya ya uzazi - Tumaini Community Services Mbeya Tanzania

Nchini Tanzania, Shirika la Tumaini Community Services linatekeleza mradi wa ‘Dreams’ yaani ‘Ndoto’ katika wilaya ya Mbeya mjini, Kyela na Mbarari mkoani Mbeya kwa ufadhili wa mfuko wa rais wa Marekani wa harakati za kupambamba na UKIMWI, PEPFAR kanda ya Tanzania, lengo likiwa kuwawezesha vijana balehe elimu ya afya ya uzazi, elimu ya kujitambua na elimu ya kiuchumi ili kupunguza maambukizi ya Virusi Vya UKIMWI.

Sauti
2'50"
UN Photo/Gregorio Cunha

UNMISS na juhudi za kupatanisha jamii za wakulima na wafugaji Magwi

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Sudan Kusini UNMISS umechukua jukumu la kuwaleta pamoja raia na vyombo vya usalama vya serikali ili kuzungumza na kusaka amani kufuatia migogoro baina ya wakulima wakazi wa Magwi na wafugaji wanaohamahama, mapigano ambayo yamesababisha vifo vya watu 130 pamoja na kuchochea vitendo vya udhalilishaji.

Sauti
2'38"
Sven Torfinn/WHO 2016

Toxorhynchites

Dokta Jovin Kitau kutoka shirika la Umoja wa Mataifa la afya ulimwenguni, WHO nchini Tanzania, ambaye ni mtaalamu wa kudhibiti na kufuatilia ugonjwa Malaria anasema Toxorhynchites wamebainika katika tafiti kuwa wanakula mbu wengine.

Sauti
1'28"
©FAO/Kenya Team

Mgeni njoo mwenyeji apone ndio hali wakulima Lodwar baada ya ujio wa WFP na FAO

Kutana na Agnes mkulima kutoka wilaya ya Lodwar kaunti ya Turkana jimbo la Rift Valley nchini Kenya. Mabadiliko ya tabianchi yanayolikumba eneo la Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa yamemuathiri sana yeye na jamii yake, lakini sasa asante kwa mradi wa pamoja wa mashirika ya Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP na la chakula na kilimo FAO wa kuwasaidia wakulima wadogo kujenga mfereji wa maji kwa ajili ya umwagiliaji na kununua mazao yao, maisha ya Agnes na jamii yake yamebadilika.

Sauti
2'36"