Asante walinda amani wanawake kwa kutujali- Wanawake Beni, DRC
Katika maadhimisho ya siku ya walinda amani duniani hii leo, maudhui yakilenga wanawake walinda amani ni ufunguo wa amani ya kudumu, baadhi ya wanawake wakazi wa mji wa Beni, jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC, wameomba walinda amani wanawake kutoka Tanzania waendelee kuwaunga mkono kiuchumi na kijamii.
Mmoja wa wanawake hao ni Kassoki Vaytsora Nadine, Chifu wa Kata ya Matembo mjini Beni ambaye msingi wa maombi yake ni changamoto wanazozipata akizitaja kuwa ni: