Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Balozi Affey mjumbe maalum kuhusu wakimbizi Somalia

Hii leo Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Filipo Grandi amemteua Balozi Mohamed Abdi Affey kuwa mjumbe wake maalum kwa masuala ya wakimbizi huko Somalia.

Taarifa ya kamishna Grandi imesema uteuzi huo utakuwa kwa kuanzia miezi sita na umezingatia msukosuko wa wakimbizi wa Somalia ambao umekuwa ukiendelea kwa zaidi ya miongo miwili na kuathiri karibu vizazi vitatu vya wasomali.

UN Photo/Elma Okic

Kikao cha 33 cha baraza la haki za binadamu chafunga pazia

Hatimaye leo Ijumaa kikao cha 33 cha baraza la haki za binadamu kimefunga pazia mjini Geneva Uswiss, kwa wito kwa nchi wanachama kuchukua hatua dhidi ya ukatili na uwajibikaji kwa wahusika.

Miongoni mwa maazimio yaliyopitishwa ni kura ya kuundwa kwa jopo la ngazi ya juu la uchunguzi nchini Burundi, kufuatia ripoti kwa baraza hilo ya machafuko yanayoendelea, yakihusishwa na uamuzi wa Rais Pierre Nkurunziza wa kusalia muhula wa tatu madarakani.

Naibu kamishina mkuu wa haki za binadamu Kate Gilmore,anasema chombo hicho kipo kwa ajili ya kutimiza matakwa ya nchi waanchama.

Ban aunda bodi kuchunguza tukio la msafara kushambuliwa Syria

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameunda bodi itakayochunguza tukio la kushambuliwa kwa msafara wa misaada ya kibinadamu huko Urum al-Kubra nchini Syria.

Tukio hilo la tarehe 19 mwezi huu lilihusisha msafara wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na shirika la hilal nyekundu la Syria, SARC ambapo watu 18 akiwemo mkuu wa ofisi ya shirika hilo huko Urum al-Kubra waliuawa.

Taarifa ya msemaji wa Umoja wa Mataifa imemnukuu Ban akisema kuwa bodi hiyo ya wajumbe kutoka Umoja wa Mataifa itachunguza mazingira ya tukio hilo la mashambulizi na kumpatia ripoti.

Mbinu za usafiri ikiwemo punda zatumika kufikisha huduma Yemen

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF pamoja na wadau wake wamekamilisha kampeni ya siku sita ya kufikisha huduma za afya na lishe kwa wahitaji nchini Yemen.

Kampeni hiyo ya kufika maeneo yasiyofikika, ilitumia vyombo mbali mbali vya usafiri ikiwemo magari, pikipiki, punda n ahata kutembea kwa miguu kuhakikisha kampeni hiyo ya nyumba kwa nyumba inafanikiwa.

WHO yasisitizia wito wa njia za kufikisha huduma Syria

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya duniani, WHO Dkt, Margaret Chan amepazia sauti yake wito wa kuwepo kwa njia salama za kuhamisha watu wanaojeruhiwa na mashambulizi yanayoendelea nchini Syria, sambamba na kufikisha vifaa vya tiba.

Katika taarifa yake ya leo, Dkt. Chan amesema zaidi ya miaka mitano tangu kuanza kwa mapigano nchini humo vita bado inasonga akigusia zaidi mji wa Aleppo ambako vituo vya afya navyo vimezidiwa uwezo.

Akizungumzia hali hiyo mbele ya waandishi wa habari, Dkt. Rick Brennan kutoka WHO amesema.

UNICEF yaimarisha ulinzi wa watoto Tanzania

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNICEF linawekeza katika kuhakikisha ulinzi wa watoto nchini Tanzania kwa kuboresha mifumo ya kisheria na sera ili kuwahusisha wadau muhimu katika jukumu hilo.

Katika makala ifuatayo Joseph Msami anamulika namna ulinzi wa watoto unavyotekelezwa katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

UN Photo/Loey Felipe

Hisia zangu kuhusu Syria ni mchanganyiko wa huzuni na hasira:O'Brien

"Sijui nianzie wapi!..Ni kwa huzuni inayotonesha na kwa kiu ya hasira isiyoweza kupoozwa, nikiripoti kwenu aibu ya kiwango cha juu, ambayo ni hali ya kibinadamu nchini Syria leo hii." Hizo ni baadhi ya hisia za Mratibu Mkuu wa Masuala ya Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa(OCHA), Stephen O’Brien , wakati wa ripoti yake mbele ya Baraza la Usalama, kuhusu hali ya kibinaadamu nchini Syria.

Upatikanaji wa mashine za kilimo ni muhimu kwa ajili ya uzalishaji na maisha ya vijijini

Kulisha idadi kubwa ya watu inyoongezeka duniani kunahitaji uboreshaji wa hali ya juu katika usalishaji wa kilimo,mikakati na mbinu muafaka hususani barani Afrika, limesema shirika la kilimo na chakula FAO.

Ripoti ya shirika hilo imesema fursa ni lazima zitoe muongozo utakaozingatia mahitaji ya wakulima wadogowadogo na zisizohitaji mtazamo wa mapinduzi ya kijani yanayoambatana na matumizi makubwa ya dawa za kilimo na pembejeo zitakazoharibu na kutishia afya na rutuba ya mashamba.

Twataabishwa na ripoti kuwa Sudan imetumia silaha za kemikali- Dujarric

Umoja wa Mataifa umesema umetaabishwa na ripoti ya kwamba serikali ya Sudan imetumia silaha za kemikali huko Jebel Marra.

Umoja wa Mataifa umesema hayo wakati msemaji wake Stephane Dujarric alipokuwa akijibu swali la mwanahabari aliyetaka kufahamu kauli ya Umoja wa Mataifa juu ya ripoti hiyo ya Amnesty International.

Dujarric amesema wana wasiwasi mkubwa juu ya taarifa hizo kwa kuwa tangu mwanzoni mwa mwaka huu, ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na muungano wa Afrika huko Darfur, UNAMID umekuwa ukiripoti ghasia huko Jebel Marra, ghasia ambazo zimeathiri raia.