Balozi Affey mjumbe maalum kuhusu wakimbizi Somalia
Hii leo Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR, Filipo Grandi amemteua Balozi Mohamed Abdi Affey kuwa mjumbe wake maalum kwa masuala ya wakimbizi huko Somalia.
Taarifa ya kamishna Grandi imesema uteuzi huo utakuwa kwa kuanzia miezi sita na umezingatia msukosuko wa wakimbizi wa Somalia ambao umekuwa ukiendelea kwa zaidi ya miongo miwili na kuathiri karibu vizazi vitatu vya wasomali.