Wahamiaji wa Kiethiopia na Kisomali wakwama Yemen IOM yaomba msaada
Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM nchini Djibouti limetoa ombi la dharura la dola Milioni Tano kwa ajili ya kuokoa maisha ya wahamiaji wa Ethiopia na Somaliawalio kwenye mazingira magumu nchini humo baada ya kushindwa kuendelea na safari ya ughaibuni.