Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Makala Maalum

Koketso Mukubani akisimama nje ya Kituo cha Matibabu cha Sediba Hope huko Tshwane, Afrika Kusini. Anasema wanaotumia dawa za kulevya wanapaswa kujumuishwa kwenye mipango na utekelekezaji wa kinga, tiba na huduma dhidi ya VVU na Homa ya ini C.
© UNODC

Simulizi Yangu: Kuishi na Homa ya Ini aina ya C nchini Afrika Kusini

Koketso Mokubane, mwanaume huyu raia wa Afrika Kusini alibainika kuwa na Homa ya Ini C. Amesimama nje ya kituo cha matibabu cha Sediba Hope kwenye kitongoji cha Tshwane. Koketso anafanya kazi ya kwenye ofisi ya Mtandao wa Watu wanaotumia dawa za kulevya nchini Afrika Kusini. Hili ni shirika lisilo la kiserikali linalopata msaada kupitia ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kukabiliana na Dawa na Uhalifu, (UNODC) kwa lengo la kutetea haki za watu wanaotumia dawa za kulevya.

Zara Bulama akiwa amebeba mmoja wa mbuzi wake aliopokea kutoka FAO katika eneo la Gongulong, Maiduguri, Nigeria, mwezi Juni 2021.
UNOCHA/Damilola Onafuwa

Katikati ya mchakato: Njia 5 zinazotumiwa na UN kuharakisha ufikiaji wa SDGs

Katika nusu ya mchakato wa hatua za kufikia ajenda kabambe ya 2030 ya Maendeleo Endelevu, nchi wanachama, wavumbuzi, na washawishi wamekusanyika katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa leo Jumatatu wakati Baraza la uchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa (ECOSOC) litakuwa linaonyesha mafanikio yaliypopatikana baada ya janga la COVID-19 katika harakati za kuelekea utimizaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), likizindua ripoti yake ya hivi karibuni ya maendeleo.