MINUSCA yachukua hatua kukabili habari potofu n aza uongo CAR
Pakua
Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR kwa muda mrefu imegubikwa na mizozo ya wenyewe kwa wenyewe hususuan maeneo ya kaskazini mwa nchi. Umoja wa Mataifa umekuwa na juhudi mbalimbali za kuleta amani hadi kuwezesha kufanyika kwa uchaguzi mwaka 2016 uliomwezesha Rais wa sasa Faustin Archange Touadera kuwa madarakani. Ingawa hivyo kumekuweko na changamoto za mivutano huku kuenea kwa habari potofu na za uongo kuwa moja ya kichocheo. Kwa kutambua hilo ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini humo, MINUSCA umechukua hatua. Je ni zipi hizo? Ungana na Assumpta Massoi kwenye makala hii.
Audio Credit
Selina Jerobon/Assumpta Massoi
Audio Duration
3'56"