Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Vijana tusipoteze matumaini bado tuna fursa ya kukabili changamoto ya tabianchi: Omesa Mukaya

Vijana tusipoteze matumaini bado tuna fursa ya kukabili changamoto ya tabianchi: Omesa Mukaya

Pakua

Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu malengo ya maendeleo endelevu HLPF linaendelea hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa ambapo wawakilishi wa nchi na serikali, wanasayansi, wanazuoni, mashirika ya umoja wa Mataifa asasi mbalimbali na vijana wanashiriki kukuna vichwa kujadili nini cha kufanyua kuhakikisha malengo hayo muhimu ya maendeleo yanatimizwa ifikpo mwaka 2030 na nini kifanyike kuzisaidia nchi zinazosuasua. Miongoni mwa washiriki ni kijana Omesa Mukaya kutoka Kenya ambaye mwezi Mei mwaka huu amehitimu shahada ya kwanza ya masuala ya sayansi ya mazingira na será katika chuo kikuu cha Clark Jimboni Massachussets hapa Marekani, amemweleza Flora Nducha wa Idhaa hii kilichomleta katika jukwaa hili.

Audio Credit
Selina Jerobon/Flora Nducha
Audio Duration
6'20"
Photo Credit
UN News