Adhabu ya wanafunzi shuleni yazua mjadala kutoka kwa wahusika Tanzania
Pakua
Upatikanaji wa elimu ni suala ambalo linaghubikwa na changamoto nyingi iwe ni kwa upande wa kufikia elimu yenyewe au pale elimu inapopatikana viwango vyake au mazingira yanayokwamisha ufikiaji wa elimu hiyo. Suala la nidhamu pia na dhamira ya wanafunzi katika kupata elimu pia ni mtihani. Hali ni kama hiyo kwa wazazi wa wanafunzi wa shule moja nchini Tanzania kama anavyosimulia John Kabambala wa Radio washirika Kids Time FM ya mkoani Morogoro nchini humo.
Sauti
3'31"