Uganda yahaha kuinua uzalishaji wa bidhaa za mifugo
Katika juhudi za kutekeleza malengo ya maendeleo endelevu au SDGs na kuinua uchumi wa taifa Uganda imeamua kuchukua hatua mathubuti katika sekta mbalimbali ikiwemo ya ufugaji. Hivi sasa kupitia ongezeko la uzalishaji wa bidhaa za mifugo kwa ajili ya mauzo nje ya nchi, Uganda imelivalia njuga suala la kuwekeza katika teknolojia za kisasa, wakati huu ambapo nchi za Ulaya na China zimefungua milango kwa kununua bidhaa za mifugo na kilimo kutoka Uganda.