Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Makala

Photo: Helga76

Tusipoelewana vyema, itakuwa ni mzozo kila wakati na watu wa asili- Bi. Mulenkei

Kila uchao Umoja wa Mataifa unapigia chepuo ahadi ya nchi wanachama 193 ya kutomwacha nyuma mtu yeyote katika utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs, ahadi iliyopitishwa na nchi hizo mwaka 2015  jijini New York, Marekani. Ahadi hiyo inazingatiwa katika utekelezaji wa malengo yote 17 na jambo la msingi  ni kwamba mtu yeyote bila kujali kabila, rangi,  umri, jinsi au imani  yake ya kidini au kisiasa, hapaswi kuenguliwa. Kama ni masuala ya afya, mazingira, elimu au uchumi basi ujumuishaji lazima uzingatiwe.

Sauti
4'33"
UNESCO

Kijana mkimbizi aanzisha radio kambini, wakimbizi wakisisitiza umuhimu wake Kyangwali, Uganda

Wakati dunia ikiadhimisha siku ya radio hii leo, shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO limsema radio inahabarisha, kubadilisha maisha na kuwaleta watu pamoja licha ya utofauti wao. Zaidi ya hayo radio ni chombo muhimu katika kukabiliana na ukatilia na kuenea kwa mizozo hususan katika maeneo kunakoshuhudiwa hali hiyo. Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa radio ni muhimu kwa watu ambao wanajikuta ukimbizini kufuatia uwepo wa ukatili au mizozo wanakotokea.

Sauti
4'
Nadhifa Zubeir

Zaidi ya kuwa mhandisi, Nadhifa Zubeir ni mama na mke

Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa, katika masomo ya ngazi ya juu takribani asilimia 30 pekee ya wanafunzi wa kike ndiyo wanachagua masomo yanayohusiana na sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati. Moja ya sababu zinazotajwa kuchangia hali hiyo ni pamoja na mfumo dume unaowafanya wasichana na wanawake kushughulika zaidi na kazi za kifamilia na hivyo kuwapa nafasi zaidi wanaume kung’ara katika masomo.

Sauti
3'19"
UN Environment

Kumalizika kwa safari ya Flip Flopi sio mwisho wa uhamasishaji kuhusu plastiki:UNEP

Dau la FlipFlopi lililojengwa na Ali Skanda kwa tani elfu 10 za taka za plastiki wiki iliyopita lilihitimisha ziara yake ya kuelimisha jamii kuhusu athari za taka za plastiki kwa siku 14. Ziara hiyo iliyoanza tarehe 24 mwezi Januari huko Lamu, nchini Kenya na kupitia Kipini, Malindi,Watamu, Kilifi, Mombasa, Diani, Shimoni, Wete, Pemba Kusini, Nungwi ilikamilika  tarehe 7 Februari katika Mji Mkongwe Zanzibar kwa mafanikio makubwa na kutimiza lengo lililokusudiwa. Lakini je kumaliza kwa safari hiyo ndio mwisho wa kupiga debe dhidi ya matumizi ya plastiki?

Sauti
3'40"
Picha/Worldreader

Kajiado ya kati nasisitiza elimu bora, sio, bora elimu- mbunge Kanchory

Ripoti ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ya hatua zlilizopigwa katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu ya mwaka 2018 inaonyesha kuwa watoto na barubaru kote ulimwenguni hawafikii viwango vya kusoma na hisibati na kwamba juhudi madhubuti zinahitajika kuimarisha viwango vya elimu.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo tofauti zinakuwa kwa misingi ya kijinsia, maeneo ya mijini na vijijini na sababu zingine ambazo zimejikita, aidha katikauwekezaji zaidi unaohitajika katika miundombinu ya elimu hususan katika nchi zinazoendelea.

Sauti
4'13"
Warren Bright/UNFPA Tanzania

Vijana wasichana na wavulana mkoani Mara wasimama kidete kukabiliana na FGM

Umoja wa Mataifa kupitia lengo namba 5 la malengo ya maendeleo endelevu, SDGs la usawa wa kijinsia, ukipaza sauti hatua zichukuliwe ili kutokomeza kitendo cha ukeketaji wa watoto wa kike na wanawake, mkoani Mara nchini Tanzania tayari hatua zinachukuliwa na zinazaa matunda. Mafunzo kwenye kituo cha ushirika wa kutokomeza ukeketaji, ATFGM kilichopo  kijiji cha Masanga yamekuwa ni chachu ya kutekeleza wito huo kwa kuwa wasichana kwa wavulana wanapata mafunzo ya kuwawezesha kuepukana na tohara na ukeketaji ambao unahatarisha maisha yao.

Sauti
4'10"
UNIC/Stella Vuzo

Mwalimu wa kike aanzisha biashara inayotoa fursa za ajira kwa wengine Uganda

Wanawake wanajumuisha takriban asilimia 52.5 ya nguvu kazi na ni kiungo muhimu katika kufanikisha melengo ya maendeleo endelevu, SDGs, hususan katika sekta ya ujasiriamali kwenye biashara ndogo ndogo na za wastani. Hata hivyo, wanawake kwa kawaida hukabiliwa na changamoto nyingi ikilinganishwa na wanaume katika kuanzisha, kusimamia na kukuza biashahra hizo kwa mujibu wa ripoti ya shirika la kazi ulimwenguni, ILO, iliyoangazia uwekezaji wa wanawake na mapendekezo nchini Uganda mwaka 2014.

Sauti
3'59"
Photo: UN/DPI Photo

Watu wa asili ni wahifadhi wa maeneo yao ya asili na si wavurugaji- Dkt. Ogada

Vuta  nikuvute kati ya watu wa jamii ya asili na wanyama imekuwa ikiendelea maeneo mbalimbali duniani ambako serikali zinataka kuhifadhi wanyama huku watu wa asili nao wakisema uasili wao unaendana na mazingira waliyomo, hivyo wanapaswa kusalia kwenye mazingira hayo. Ni kwa kuzingatia mvutano huo hivi karibuni wakati wa mkutano wa jopo la wataalamu wa masuala ya watu wa jamii za asili huko Nairobi, Kenya, Newton Kanhema wa kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa nchini humo, UNIC Nairobi, alimsaka Dkt.

Sauti
4'24"