Waliofurushwa makwao Iraq wahaha kwa mapigano zaidi na baridi
Watu wapatao 400,000 nchini Iraq hawana makazi ya kutosha huku wengine 780,000 wakiishi bila bidhaa muhimu za nyumbani na za kuendeleza ubora wa maisha yao wakati huu wa msimu wa baridi kali, limesema Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuratibu Masuala ya Kibinadamu, OCHA.
Kwa mujibu wa OCHA, serikali ya Iraq na wadau wa kitaifa na kimataifa wanaoa usaidizi wa vifaa vya kupasha moto mahema, nguo za joto, fedha, mafuta na vifaa vingine vya kuboresha hali ya maisha.