Wakazi wa Cabo Delgado nchini Msumbiji hatihati kukosa misaada ya binadamu iwapo WFP haitapatiwa fedha za nyongeza
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani, WFP linasema iwapo halitapokea fedha za nyongeza, litalazimika kusitisha msaada muhimu wa kibinadamu kwa wakazi milioni moja wa jimbo la Cabo Delgado nchini Msumbiji ifikapo kilele cha msimu wa njaa mwezi Februari mwakani kutokana na ukata unaokabili. Leah Mushi na taarifa zaidi.