Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Habari kwa Ujumla

Umoja, Mshikamano wa Pamoja ndiyo Njia Bora ya Kutanzua mzozo wa Guinea-Bissau

Mwanadiplomasia wa Umoja wa Mataifa amependekeza hatua zinazopaswa kupitiwa ili kutafutia majawabu mzozo wa kisiasa uliolikumba taifa la Guinea-Bissau lililopo katika pembe ya Afrika Magharibi ambalo hivi karibuni lilishuhudia mapinduzi ya kijeshi.

Taifa hilo hata hivyo linahistoria ya kukumbwa na matukio ya wanajeshi kupoka madaraka tangu lilipojipatia uhuru wake mwaka 1974 toka wa Ureno.