Radio Sauti ya Injili Goma yatumia Kiswahili kusongesha amani DRC
Pakua
katika kukuza lugha ya Kiswahili duniani Baraza la Kiswahili la Taifa nchini Tanzania BAKITA limeandaa kongamano la wiki moja la Idhaa za Kiswahili duniani na kuwakutanisha wadau kutoka nchi mbalimbali zinazozungumza lugha ya Kiswahili jijini Arusha nchini humo.
Stella Vuzo wa Kituo cha habari cha Umoja wa Mataifa UNIC Dar es Salaam, Tanzania anashiriki Kongamano hilo na amefanya mahojiano na Mkurugenzi wa Redio sauti ya Injili iliyoko Goma jimboni Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia Kongo -DRC Mchungaji Ezra Kasereka Makoma anayeanza kwa kueleza namna redio yao inavyofundisha lugha ya Kiswahili wananchi wa DRC na nchi jirani ya Rwanda.
Audio Credit
Assumpta Massoi/Stella Vuzo
Audio Duration
3'45"