Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Katu mtu asilazimishwe kujiunga na chama hata ndani ya familia- Wakili Komba

Katu mtu asilazimishwe kujiunga na chama hata ndani ya familia- Wakili Komba

Pakua

Tamko la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa ambalo mwaka  huu linatimiza miaka 70 tangu kuasisiwa lina ibara 30 ambazo ni msingi wa haki za binadamu kote duniani. Licha ya kuwepo kwa muda mrefu baadhi ya haki zinasiginwa katika baadhi ya maeneo na sababu kuu ni kwa wanachi kutofahamu vyema haki zao. Ni kwa msingi tumekuwa tunakuletea uchambuzi wa Ibara kwa Ibara ambapo leo Wakili Aloyce Komba kutoka Tanzania amezungumza na Arnold Kayanda wa Idhaa hii akifafanua ibara ya 20. Ibara hii ina sehemu mbili ambapo sehemu ya kwanza inasema kila mtu ana haki na uhuru wa kukusanyika na kujiunga na kikundi ilhali sehemu ya pili inasema hakuna mtu anayepashwa kulazimishwa kujiunga na kikundi chochote. Wakili Komba anaanza kwa kufafanua kwa muhtasari ibara ina maana gani.

 

Audio Credit
Grace Kaneiya/Arnold Kayanda
Audio Duration
4'18"
Photo Credit
Maandamano huko DRC mwezi Disemba mwaka 2016. (Picha:MONUSCO)