Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bajeti za nchi zizingatie ustawi wa wanawake: Kikwete

Bajeti za nchi zizingatie ustawi wa wanawake: Kikwete

Pakua

Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema wanawake hawajengewi mazingira ya kutosha ya ustawi wa kijamii na  kiuchumi kama ilivyo wanaume hususani katika nchi zinazoendelea akitolea mfano wa bajeti za serikali ambazo hazizingatii ukuaji nwa kundi hilo. Katika mahojiano maalum na Joseph Msami wa idhaa hii muda mfupi baada ya kuhutubia mjadala kuhusu kupambana na ukosefu wa usawa na kuwezesha wanawake na wasichana ikiwa ni sehemu ya malengo ya maendeleo endelevu SDGs, Rais Kikwete anataja mambo kadhaa ambayo ni muhimu kwa wanawake ikiwamo elimu.

Photo Credit
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania akihojiwa na Joseph Msami wa Radio ya Umoja wa Mataifa. (Picha:UN-Idhaa ya Kiswahili/Assumpta Massoi)