Vijana Tanzania kunufaika na siku ya idadi ya watu:UNFPA
Pakua
Tarehe 18 Novemba kila mwaka ni siku ya kimataifa ya idadi ya watu. Siku hii hutumiwa kufahamu idadi ya watu duniani na huku takwimu hizo zikitumiwa kupanga mikakati ya ustawi wa watu duniani kote. Maudhui ya siku hiyo mwaka huu ni ustawi wa vijana kundi ambalo ni nguvu kazi katika jamii.
Shirika la idadi ya watu duniani UNFPA ndilo linaloratibu kazi hiyo ambapo nchini Tanzania shirika hilo hilo linatarajia kuitumia siku hiyo kuwanufaisha vijana. Katika mahojiano na afisa mawasiliano wa UNFPA Tanzania Sawiche Wamunza, afisa wa idadi ya watu na maendeleo
Samweli Msokwa anaanza kwa kueleza kauli mbiu ya siku hiyo.
(SAUTI MAHOJIANO)