Wakimbizi Iraq wahangaika kujiandaa kwa majira ya baridi kali
Pakua
Juhudi zinaendelea sasa nchini Syria, Iraq na nchi jirani, kuwaandaa wakimbizi wa kigeni na wa ndani kwa msimu wa baridi.
Lakini watu milioni moja waliolazimika kuhama makwao Syria na Iraq, na kwingineko katika ukanda hawataweza kupata usaidizi kwa sababu ya upungufu wa dola milioni 58.4 za ufadhili kwa ajili ya mipango ya majira ya baridi.
Ungana na Joshua Mmali katika Makala hii, inayomulika hali wanayokabiliana nayo baadhi ya wakimbizi hao.