Kilimo cha mpunga chaboreshwa Zanzibar kupitia nguvu za kiatomiki
Pakua
Shirika la Kimataifa la Nguvu za Atomiki, IAEA, linatumia miyonzi ya nyuklia kuboresha mbegu za mazao mbalimbali na kuimarisha kilimo katika nchi zinazoendelea.
Mbegu hizo bora zinasaidia kustahimili ukame na wadudu mbalimbali na kuongeza mavuno ya mazao hayo. mfumo huo umeleta mabadiliko makubkwa kwenye jamii ya wakulima, katika wilaya ya Kaskazini A, kisiwani cha Zanzibar, Tanzania. Ungana na Priscilla Lecomte kwenye makala hiyo!