28 AGOSTI 2023
Hii leo jaridani jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Zimbabwe baada ya uchaguzi na masuala ya afya nchini Botswana. Makala tunakupeleka nchini Mali na mashinani nchini Rwanda, kulikoni?
Hii leo jaridani jaridani tunaangazia hali ya usalama nchini Zimbabwe baada ya uchaguzi na masuala ya afya nchini Botswana. Makala tunakupeleka nchini Mali na mashinani nchini Rwanda, kulikoni?
Mwaka mmoja tangu mafuriko ya kihistoria yakumbe Pakistani, na hali ya dharura nchini humo kutangazwa, mamilioni ya watoto bado wanaendelea kuhitaji misaada ya dharura huku operesheni za ukarabati zikisalia kukumbwa na ukata kwani fedha zinazotakiwa hazijapatikana.
Vita inayoendelea nchini Sudan inachochea dharura kubwa ya kibinadamu ambapo vita na njaa, magonjwa na watu kufurushwa makwao vilivyofuatia sasa inatishia ‘kutafuna’ nchi nzima, amesema Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA, Martin Griffiths.
Hii leo jaridani jaridani tunaangazia haki za binadamu nchini Sudan na utaifa wa Wapemba nchini Kenya. Makala tunakupeleka nchini Pakistan na mashinani nchini Tanzania, kulikoni?
Mwishoni mwa mwezi uliopita Rais wa Kenya William Ruto akiwa Kilifi mashariki mwa Kenya alitangaza kutambulika rasmi kwa jamii ya Wapemba ambao kwa miaka mingi waliishi nchini humo wakikosa hadhi ya utaifa kwa kuwa vizazi vyao vya nyuma vilitoka nje ya Kenya.
Katika kujifunza lugha ya Kiswahili Dkt. Mwanahija Ali Juma, Katibu Mtendaji wa Baraza la Kiswahili Zanzibar, BAKIZA nchini Tanzania anachambua methali, "Mnywa Maji kwa Mkono Mmoja Kiu yake I pale pale."
Ikiwa imesalia takribani miaka 6 ushehe kufika mwaka 2030 muda ambao ulimwengu ulijiwekea lengo la kuwa umetimiza Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs), mapema mwaka huu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akiamini wanawake wanasayansi wana uwezo wa kuchangia haraka katika maendeleo ya ulimwengu, alie
Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina na Mwanaisha Ulenge ni Mwanamke Mwanasayansi Mhandisi, Mbunge nchini Tanzania vilevile Mjumbe wa Shirikisho la Mabunge Duniani (IPU) na hivi karibuni akiwa katika ziara ya kikazi hapa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa Anold Kayanda alipata fursa ya
Maadhimisho ya Wiki ya Maji yakiendelea huko Stockholm nchini Sweden, shirika la Umoja wa Mataifa la Mazingira duniani, (UNEP) leo limezindua ripoti yenye lengo la kugeuza majitaka kuwa jawabu la uhaba wa maji na changamoto ya tabianchi duniani.
Hii leo jaridani tunaangazia wiki ya maji na kazi ya Umoja wa mataifa katika utoaji wa huduma za maji. Makala tunakuletea uchambuzi wa Ibara ya 8 ya Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu na mashinani tunakupeleka jijini Mbeya nchini Tanzania, kulikoni?