Mlipuko wa nzige wa jangwani Yemen na pembe ya Afrika waweza kuwa hatari-FAO
Shirika la chakula na kilimo FAO leo limetoa onyo dhidi ya mlipuko wa nzige wa jangwani katika eneo la Pembe ya afrika na Yemen, likisema nzige hao waliochochewa na mvua kubwa wanaweza kuwa tishio kubwa kwa uzalishaji wa kilimo katika miezi mitatu ijayo