Baraza la Usalama lalaani mashambulizi ya kigaidi Kyrgystan.
Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wamelaani vikali shambulio la bomu dhidi ya ubalozi wa China huko Kyrgyzstan.
Shambulio hilo la tarehe 30 Agosti kwenye mji mkuu, Bishkek, lilisababisha majeraha kwa wafanya kazi wa ubalozi huo.