O’Brien atoa wito usaidizi uongezwe kwa Wasyria wenye uhitaji
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu, ambaye pia ni mratibu wa misaada ya dharura (OCHA), Stephen O’Brien, ametoa wito usaidizi zaidi utolewe kwa Wasyria wenye uhitaji ndani ya Syria na katika ukanda mzima wa Mashariki ya Kati.