Betty Koliri kwenye boda boda ni Afisa Ustawi wa Jamii kaunti ya Kaabong nchini Uganda. Hapa anaelekea kumtembelea mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 16 aliyetekwa na kulazimishwa kuolewa lakini hatimaye ameokolewa. Kwa msaada mtuhumiwa alikamatwa, akafunguliwa mashtaka na kuhukumiwa kifungo cha miaka 7 jela na manusura amerejea shuleni.
Brenda Nabiriye Naibu Kiranja Mkuu shule ya sekondari ya Mpumudde nchini Uganda anasema iwapo wazazi hawatozungumza na watoto wa kike kuhusu hatari ya ukatili wa kingono, watoto hao wataendelea kuwa hatarini. Wazazi lazima wawe marafiki bora kwa watoto wao ili waelezane ukweli.
Mable Achom, Kiranja Mkuu wa shule ya sekondari ya wasichana ya Wangange nchini Uganda akitia saini kwa niaba ya wanafunzi wenzake kushirikiana na wadau kushughulikia ulawiti wa watoto, ndoa za utotoni na mimba za utotoni. Kwa mujibu wa UNFPA, takribani watoto wa kike1,052 hupata ujauzito kila mwaka nchini Uganda.
Mtoto ambaye alinusuriwa na wenzake sita kukeketwa baada ya kuvushwa mpaka hadi Kenya. Ingawa mama na bibi yangu wamekeketwa, mimi sitaki, nataka nifuate njia yangu. Sasa anasoma darasa la Kwanza shule ya msingi ya wasichana ya Kalas wilaya ya Amudat nchini Uganda.