Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

KM anashtushwa na uhasama wa Eritrea dhidi ya UM

Kufuatia uamuzi wa Serekali ya Eritrea kupiga marufuku na kuwafukuza watumishi watano wa Umoja wa Mataifa, Katibu Mkuu amelazimika kutoa malalamiko juu ya tabia ya uhasama uliolivaa taifa hilo dhidi ya Shirika la Ulinzi wa Amani la UM Mipakani kati ya Ethiopia na Eritrea (UNMEE), shirika ambalo mtumishi wake mmoja alikamatwa hivi karibuni na Eritrea na kuwekwa kizuizini.

Fafanuzi za FAO juu ya Malengo ya MDGS

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo Duniani (FAO), Bw Jacques Diouf ameonya ya kuwa jumuiya ya kimataifa haitofanikiwa kukamilisha kwa wakati Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) bila ya kukabiliana, kama inavyopaswa, na tatizo liliokithiri la njaa na umaskini.

Serikali ya Somalia kuanza mazungumzo ya amani mjini Khartoum

Wajumbe wa serekali ya mpito ya Somalia na wale wa Baraza la mahakama ya kiislamu linalodhibiti mji mkuu wa Mogadishu na sehemu kubwa ya nchi, wanaanza duru ya pili ya mazungumzo ya amani mjini Khartoum hii leo. Abdushakur Aboud amezungumza na mbunge na waziri mdogo wa zamani Hussein Bantu huko Baido na kumuliza kwanza mazungumzo yatahusu masuala gani. ~~