WEIF2024 yaanza Bahrain ikilenga kuchochea ugunduzi na ujasiriamali
Jukwaa la tano la kimataifa la uwekezaji kwa ujasiriamali, WEIF2024 linaloungwa mkono na Umoja wa Mataifa limeanza leo huko Manama, Bahrain likiwa na wawakilishi wa serikali, mashirika ya kiraia, wawekezaji, wasomi na wabunifu na wakitoka pembe zote za dunia kwa lengo la kusaka mbinu za kuchochea ubunifu na ugunduzi ili hatimaye kusaidia kusongesha malengo ya maendeleo endelevu.