Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Mtoto akiwa juu ya lundo la mchanga ambao hutumiwa na wakazi wa eneo hili kujaribu kuzuia maji ya ziwa Albert yasiingie kwenye makazi yao.
UN/ John Kibego

Waandishi wa habari 44 waliuawa wakichunguza masuala ya mazingira

Hii leo ni siku ya kimataifa ya uhuru wa vyombo vya habari maudhui yakiwa Uandishi wa Habari wakati huu wa janga la mazingira ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kwa kushirikiana na shirikisho la waandishi wa habari duniani, IFJ wametoa ripoti yao ikionesha kuwa ni katika kipindi cha miaka 15 iliyopita waandishi wa habari 44 waliuawa wakiwa wanachunguza masuala ya mazingira. Kampeni ya siku hii ni kwamba kila habari kuhusu mazingira lazima isimuliwe hivyo waandishi wa habari walindwe.

Kaskazini mwa Gaza iko kwenye magofu baada ya miezi kadhaa ya mashambulizi ya mabomu.
© WFP/Ali Jadallah

Wananchi wa Gaza wako katika jakamoyo wakisubiri taarifa kuhusu wito wa kusitisha mapigano: UN

Wakati kukiwa na ongezeko la wito wa kimataifa kwa Israel kujizuia na mashambulizi zaidi Gaza na ripoti za leo za mashambulizi mengine mabaya zaidi ya usiku kucha, wahudumu wa kibinadamu wa Umoja wa Mataifa wamesisitiza kuhusu athari mbaya zinazoendelea za vita hiyo na haja ya kuhakikisha njia za kuaminika za usambazaji wa misaada kwa watu wanaohitaji kwa udi na uvumba zinapatikana. 

Audio Duration
1'57"