Guterres apongeza ASEAN kwa kujenga madaraja ya maelewano duniani
Mivutano ya kisiasa na kijiografia ikiendelea kushamiri duniani, ukanda wa Kusini-Mashariki mwa bara la Asia unatekeleza dhima muhimu ya kujenga madaraja ya maelewano duniani kote, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa hii leo huko Jakarta, Indonesia.