Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

ASEAN

07 SEPTEMBA 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo Magavana Dkt. Wilber Ottichilo wa Kaunti ya Vihiga na Gavana wa Kaunti ya Narok, Patrick Ole Ntutu hivi karibuni walipohudhuria Jukwaa la ngazi ya juu la kisiasa kuhusu SDGs lijulikanalo kama HLPF hapa katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, waliketi na Flora Nducha wa Idhaa hii ya Kiswahili ya Umoja wa Mataifa ili waeleze mipango yao ya kutimiza Malengo ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo Endelevu, SDGs katika majimbo yao huko nchini Kenya.

Sauti
9'58"
UN

Asante Mungu angalau tumepata chakula- Wasema wakazi wa Belet Weyne

Umoja wa Mataifa umeunga mkono juhudi za Somalia za kusambaza misaada ya dharura kwa makumi ya maelfu ya wananchi walioathiriwa na mafuriko hususan kwenye wilaya ya Belet Weyne jimboni Hirshabelle. Grace Kaneiya na ripoti kamili.

Mafuriko katika jimbo la Hirshabelle yameleta tafrani kubwa, nyumba zikitwama na wakazi kushindwa kujipatia huduma muhimu ikiwemo chakula.

Sauti
2'13"