Nchini Zimbabwe, kitendo cha vikosi vya usalama kutumia nguvu kupita kiasi ikiwemo risasi za moto kudhibiti waandamanaji wanaopinga hali nguvu ya uchumi na kijamii, ikiwemo kuongezeka kwa bei ya mafuta, kimesababisha ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa itoe tamko la kuelezea wasiwasi wake juu ya mwelekeo wa hatua hiyo.