Chuja:

zambia

12 Agosti 2021

Ikiwa leo ni siku ya vijana duniani, Umoja wa Mataifa unapigia chepuo ushiriki wa vijana katika kuimarisha mifumo ya chakula duniani kwa kuzingatia kuwa miaka 30 ijayo watu bilioni 2 zaidi wataongezeka duniani na kuongeza mahitaji ikiwemo ya chakula.

Nchini Zambia wanufaika wa mradi wa kuimarisha lishe au SUN ulioanza mwaka 2014 wamepaza sauti zao wakielezea jinsi watoto wao wameimarika kiafya na wakati huo huo kipato cha familia kuongezeka.

Sauti
12'11"

23 Februari 2021

Hii leo jaridani Flora Nducha anaanzia na ripoti mpya ya shirika la kazi la Umoja wa Mataifa, ILO ikiangazia majukwaa mapya ya ajira duniani yakiwemo yale ya mtandaoni na faida na changamoto zake. Kisha anakwenda nchini DR Congo ambako kikongwe mmoja amekata tamaa ya maisha baada ya kufurushwa kwake mara tatu. Taarifa nyingine ni kutoka Lebanon ambako theluji pasi kifani yatishia maisha ya wakimbizi. Makala anabisha hodi mkoani njombe nchini Tanzania mtaalamu wa lishe anazungmzia faida za mboga na matunda.

25 Januari 2021

Hii leo mwenyeji wako Grace Kaneiya akiwa Nairobi Kenya anajikita katika mada kwa kina kutoka Zambia ambako shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF linasaidia jimbo la Luapula kuwa na huduma za maji safi na kujisafi. Mashinani anasalia huko huko Kenya na mtoto akizungumzia masomo yalivyorejea sasa baada ya shule kufungwa kutokana na COVID-19 lakini pia kuna habari kwa ufupi. Karibu!

Sauti
10'27"