Uchunguzi kuhusu COVID-19 wahimiza ujasiri wa hatua za kuzuia janga hilo:WHO
Jopo la ngazi ya juu lililoteuliwa na Shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO, leo limehimiza kuchukuliwa hatua za kijasiri ili kumaliza janga la corona au COVID-19, huku pia likitaka shirika hilo la Umoja wa Mataifa lipewe mamlaka zaidi ya kuchukua hatua za haraka zaidi kwa vitisho vya siku zijazo vya milipuko ya majanga kama hili.