Umoja wa Mataifa umeeleza kusikitishwa na kuongezeka kwa machafuko na mateso kwa raia wa Sudan Kusini, kufuatia operesheni ya hivi karibuni ya jeshi serikali ya nchi hiyo.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na kuzuia mauaji ya kimbari na wajibu wa kulinda, imekuwa na mjadala leo na nchi wanachama kuhusu suala hilo, kama sehemu ya maandalizi ya ripoti ya Katibu Mkuu kuhusu wajibu wa kulinda.
Licha ya kutokuwepo na hali ya hewa ya El Niño hadi sasa mwaka huu , kuna uwezekano mkubwa wa zaidi ya asilimia 50 hali hiyo itajitokeza katika nusu ya pili ya mwaka huu wa 2017.