Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa leo kwa mara nyingine limetoa wito kwa pande zinaziohusiaka katika vita kuchukua hatua za kuwalinda raia kutokana na athari za machafuko.
Mwakilishi maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia amelitaka bunge la mpito la nchi hiyo kulikubali baraza jipya la mawaziri kwa kile alichokiita njia ya kuelekea amani ya taifa hilo la pembe ya Afrika.
Nchi ambazo zimeunga mkono mkataba wa Umoja wa Mataifa juu ya upigaji marafuku wa matumizi ya tumbaku zimepitisha mpango mpya wenye lengo kuongeza nguvu ili kukabiliana na matumizi ya tumbaku duniani.
Majimbo yote ya Iraq jana Jumapili yameanza siku kumi za maadhimisho ya sherehe za siku ya kimataifa ya watoto ambapo tarehe 21 Novemba ni siku ya maadhimisho ya mkataba wa haki za mtoto.
Shirika la Umoja wa mataifa linalopambana na maradhi ya ukimwi UNAIDS limekaribisha matamshi ya baba Benedict wa kumi na sita kuwa matumizi ya mipira ya kondomu kuzuia maambukizi ya ukimwi yanakubalika .
Kesi ya aliyekuwa kiongozi wa kundi la waasi nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Jean Pierre Bemba imeanza kusikilizwa leo kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu ya ICC mjini the Hague Uholanzi.
Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa gharama za matibabu zinaendelea kuwa ghali na kusababisha mamilioni ya watu na hata kutoka mataifa yaliyostawi kuwa maskini.
Serikali ya Burundi imesema vikosi vyake vya kulinda amani vilivyojumuishwa kwenye vikosi vya muungano wa Afrika AMISOM nchini Somalia visalia endapo tuu msaada na mahitaji muhimu yakipatikana.