Mkutanao mkuu wa UM, wa siku tatu unaozingataia udhibiti bora wa akiba ya chaklula duniani, umefunguliwa rasmi leo hii kwenye mji wa Roma, Utaliana ambapo KM Ban Ki-moon, kwenye risala yale alionya kwa kukumbusha mnamo siku ya leo pekee watoto 17,000 watafariki duniani kwa sababu ya kusumbuliwa na njaa - ikijumlisha kifo cha mtoto mmoja katika kila nukta tano za dakika - jumla ambayo kwa mwaka inakadiriwa kukiuka vifo milioni 6 vya watoto, licha ya kuwa sayari yetu imebarikiwa chakula cha kuweza kutosheleza mahitaji ya chakula kwa umma wote wa kimataifa, alisisitiza KM.