Wiki hii Naibu KM Asha-Rose Migiro alipata fursa ya kuzungumzia suala la udhalilishaji wa kijinsia, kwenye mkutano maalumu uliotayarishwa mjini New York na Halmashauri ya Mataifa ya Ulaya pamoja na Ubalozi wa San Marino katika UM. Kwenye risala alioitoa mbele ya kikao hicho NKM Migiro alihimiza kuchukuliwe hatua za pamoja, kukomesha haraka tabia ya utumiaji nguvu na mabavu dhidi ya wanawake, hatua ambayo ikikamilishwa, alitilia mkazo, itawavua wanawake na mateso hayo maututi.~