Kamisheni ya UM juu ya Haki ya Wanawake Duniani (CSW)ilikusanyisha wajumbe kadha wa kadha wa kimataifa, kwenye Makao Makuu ya UM, waliohudhuria kikao cha mwaka, cha 52, ambapo kuanzia tarehe 25 Februari hadi Machi 07, 2008 wajumbe hawa walizingatia kipamoja yale masuala yanayohusu haki za wanawake.