Dktr Margaret Chan, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) alihimiza viongozi na wajumbe waliohudhuria kikao cha mwaka cha sita cha bodi linaloandaa sera na miradi ya afya ya kimataifa, kinachokutana hivi sasa Geneva, Uswiss kwamba kunatakikana hima kuu ya jumla kutoka kwao wote, kujenga kile alichokiita “urithi wa afya”, kadhia ambayo alitumai ikikamilishwa itasaidia kuaboresha siha za wanawake na afya ya umma wa Afrika, kwa ujumla; kwa sababu, Dktr Chan anaamini kidhati kuwa wanawake ni fungu muhimu la umma wa kimataifa, linaloongoza kwenye harakati kadha wa kadha za maendeleo ulimwenguni.