Akizungumza na Redio ya Umoja wa Mataifa, Christopher Mwaijonga mwakilishi mkazi msaidizi huko Tanzania, amesema kwamba, wakati wa mkutano wa Cairo juu ya Idadi ya Watu, 1994, wajumbe walisisitiza juu ya kuwekea mkazo juu ya kuwapatia uwezo wanawake kuamua wakati wanapotaka kupata mimba na kuimarisha afya ya uzazi.