Shirika la UM juu ya Mfuko wa Kudhibiti Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) imetangaza ya kuwa mwimbaji wa Tanzania, Stara Thomas, aliye maarufu katika ulimwengu unaozungumza Kiswahili, atatumia ujuzi wake wa kisanii kwa kushirikiana na UM katika huduma za kusaidia mama waja wazito nchini kwao na katika bara la Afrika kujikinga dhidi ya vifo vya katika uzazi na vifo vya watoto wachanga.