Umoja wa Mataifa na mashirika mengine ya misaada leo wameanza kupeleka msaada muhimu wa kibinadamu kwa wakimbizi wa ndani wanaohifadhiwa nje ya eneo la mpango wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika Darfur UNAMID baada ya kuondolewa vikwazo vyote vya usafiri wa anga na barabara kwenye maeneo yaliyoghubikwa na machafuko karibuni.